Kasi ya utekekezaji wa Mradi wa BOOST yawakosha Kamati ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo inayongozwa na mwenyekiti wake Mh. Husna Juma Sekiboko.



Kamati hiyo iko katika ziara ya kukagua miradi hiyo ambapo leo Septemba 10 wametembelea na kukagua ujenzi wa Shule ya Mkondo wa Kingereza ya Richard Mgana inayojengwa na mradi kwa Shilingi za Kitanzania 475,300,000 Kigogo Jijini Dar es salaam.



Shule hiyo ikikamilika inatarajia kuchukua Wanafunzi 720 kutoka maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam.