Mawaziri kutoka nchi 19 barani wameshiriki kikao  Ministerial Roundtable katika Kongamano la 18 la e-Learning Africa 2025 lililoanza Aprili 7, 2025 JNICC jijini Dar es Salaam.

Kikao hicho linalenga kujadili mikakati mbalimbali ikiwemo kuandaa rasilimaliwatu yenye maarifa na  ujuzi pamoja na kuhamasisha  matumizi ya teknolojia za kidijitali katika sekta mbalimbali hususan elimu.